Breaking News

TANESCO KWA KUSHIRIKIANA NA MKANDARASI ABB TOKA SWITZERLAND KUFUNGA TRANSFOM YENYE MEGAWITI 240


2Wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) kwa kushirikiana na Mkandarasi ABB wa nchini Switzerland, pichani wakiendelea na kazi ya kufunga Transfoma yenye uwezo wa Megawati 240 katika Kituo Kikuu cha Kupoza na Kusambaza umeme cha Ubungo.
1
Transfoma hiyo iliingia hapa nchini mnamo Januari 28, 2019 kwa nia ya kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuleta ufanisi katika usambazaji wa umeme katika jiji la Dar es Salaam na Pwani.index
Akielezea uwezo wa Transfoma hiyo, Mkuu wa Kituo cha Kupoza na Kusambaza umeme Ubungo, Mhandisi Joseph Msumali amesema Transfoma hiyo yenye uwezo wa kusukuma takribani Megawati 240 kutoka kwenye msongo wa kilovoti 220 kuelekea Msongo wa kilovoti 132 kwa ajili ya usambazaji na matumizi ya nishati ya umeme katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

No comments