Mtanzania aeleza alivyonusurika ajali ya ndege

Baada ya taarifa za ndege aina ya Boeing 737 ya Shirika la Ndege la Ethiopia ambayo ilikuwa na watu 157, kuanguka muda mfupi baada ya kupaa, na watu wote waliopo kwenye ndege hiyo kupoteza maisha, raia mmoja wa Tanzania ameeleza namna alivyopishana na ajali hiyo.
Kufuatia taarifa hiyo, Mtanzania, Antu Mandoza ambaye pia ni mjasiriamali wa urembo na tasnia ya habari, ameeleza namna alivyonusurika katika ajali hiyo iliyotokea asubuhi ya leo.
Katika ukurasa wake wa Twitter amesema kuwa alinusurika kukata tiketi katika ndege hiyo kabla ya kubadili safari ya Addis Ababa na baada ya kushuka ndipo alipokutana na taarifa hizo mbaya huku akipokea ujumbe mwingi na simu kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki waliotaka kujua hali yake.
Pata habari motomoto na za uhakika kila siku kila zinapojiri katika nyanja mbalimbali ikiwemo Siasa, Michezo, Ajira, uchumi, Mapenzi, Udaku/Umbea n.k .Kwa kudownload APP hii Bofya HAPA Kudownload.
BOFYA HAPA
No comments