Breaking News

NKANA MABINGWA MARA MBILI MFULULIZO NGAO YA JAMII:



Timu ya Nkana fc imefanikiwa kutwaa  kombe la ngao ya jamii Inayofahamika kama [ Samuel’ Zoom’ Ndhlovu Charity ] baada ya kuifunga Zesco utd kwa  mikwaju ya penati 5-4 kufuatia mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 1-1 katika mchezo huo unaoashiria ufunguzi wa ligi ya Zambia inayofahamika kama Super league.
.
. -Ligi hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi hapo kesho kwa michezo kadhaa kuchezwa ambapo pia  ikumbukwe ligi hiyo imegawanywa katika makundi mawili ,  kundi A na  kundi B huku Zesco ikiwa impangwa kundi A na Nkana red devils ikiwa imepangwa kundi B.
.
.
Bao la Zesco utd limefungwa na
Maybin Kalengo  dakika ya 2 huku bao la nkana likifungwa na  Ronald Kampamba dakika ya 46

No comments