Breaking News

Taarifa kuhusu kuanza kwa vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge Jijini Dodoma tarehe 11 hadi 31 Machi, 2019.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

BUNGE LA TANZANIA

Simu: +255 026 23222761-5

Fax No. +255 026 2322624

E-mail: info@bunge.go.tz

Ofisi ya Bunge,

S.L.P. 941,

DODOMA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUANZA KWA

VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE TAREHE 11 HADI 31

MACHI, 2019, MJINI DODOMA

_________

1.0 UTANGULIZI

Kamati za Kudumu za Bunge zitaanza kukutana Jumatatu tarehe 11

hadi 31 Machi, 2019 Mjini Dodoma kutekeleza majukumu ya

kibunge kabla ya Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge

uliopangwa kuanza tarehe 02 Aprili, 2019. Kwa mujibu wa Ratiba

ya Shughuli za Kamati, Waheshimiwa Wabunge wote wanapaswa

kuwasili Mjini Dodoma Jumapili tarehe 10 Machi, 2019 tayari kwa

ajili ya kuanza kwa vikao vya Kamati.

Shughuli zitakazotekelezwa na Kamati hizo ni pamoja na:

a) KUPOKEA WASILISHO LA SERIKALI KUHUSU KIWANGO CHA

UKOMO WA BAJETI

Katika kipindi hicho cha vikao vya Kamati za Bunge, siku ya

tarehe 12 Machi 2019, Wabunge watapokea Wasilisho la

Mapendekezo ya Serikali kuhusu Mpango na Kiwango cha Ukomo wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 kwa mujibu

wa Kanuni ya 97 ya Kanuni za Bunge Toleo la Januari, 2016.

b) KUFANYA ZIARA ZA UKAGUZI WA MIRADI

Kamati zitafanya ziara za ukaguzi wa miradi ya Maendeleo

iliyotengewa fedha katika Bajeti ya mwaka 2018/2019 kwa

mujibu wa Kanuni ya 98(1) ya Kanuni za Bunge Toleo la

Januari, 2016. Kamati zitakagua miradi ya uwekezaji

liyotekelezwa na Serikali kupitia Mashirika ya Umma. Aidha,

Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Hesabu za

Serikali za Mitaa (LAAC) zitafanya ziara za ukaguzi wa miradi

mingine iliyotekelezwa na Serikali ili kulinganisha matokeo ya

utekelezaji na thamani halisi ya fedha za Umma zilizotumika

katika miradi hiyo.

c) KUFANYA UCHAMBUZI WA BAJETI

Katika vikao hivyo pia Kamati zitafanya uchambuzi wa Taarifa

za Utekelezaji wa Bajeti za Wizara inazozisimamia kwa Mwaka

wa Fedha unaoishia 2018/2019 kwa ajili ya kufanya ulinganisho

kuhusu makadirio ya matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa

Fedha 2019/2020 kwa mujibu wa Kanuni ya 98(2) ya Kanuni za

Kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016.

d) KUFANYA UCHAMBUZI WA TAARIFA ZA UWEKEZAJI

Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) itafanya

uchambuzi wa Taarifa za Uwekezaji uliofanywa na Serikali

kupitia Mashirika ya Umma kwa mujibu wa Kifungu cha 12

cha Nyongeza ya Nane ya Kanuni za Bunge Toleo la Januari,

2016.




e) UCHAMBUZI WA SHERIA NDOGO

Kamati ya Sheria Ndogo itafanya uchambuzi wa Sheria

Ndogo zilizowasilishwa wakati wa Mkutano wa Kumi na Nne

Bunge kwa mujibu wa Kifungu cha 11 cha Nyongeza ya Nane

ya Kanuni za Bunge Toleo la Januari, 2016

Ratiba zote za Shughuli za Kamati za Bunge ikiwa ni pamoja na

maeneo ambayo Kamati hizo zitafanya ziara zinapatikana katika

Tovuti ya Bunge ambayo ni www.parliament.go.tz. mara baada ya

Kamati hizo kuanza kazi.

Imetolewa na: Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa.

Ofisi ya Bunge

DODOMA

05 Machi, 2019

No comments