Breaking News

Yanga chupuchupu Mkwakwani


Klabu ya Yanga imeshindwa kuondoka na pointi tatu kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Coastal Union baada ya kutoka sare ya bao 1-1.

Katika mchezo huo Timu ya Coastal Union ilikuwa ya kwanza kuandika bao kupitia kwa Haji Ugando dakika ya 30 na Yanga wakasawazisha kupitia kwa Matheo Anthony dakika ya 76.

Coastal Union walikumbana na pigo kwa mshambuliaji wake Issa Abushehe kutolewa nje kwa kadi nyekundu, na dakika moja baadaye Yanga wakasawazisha

No comments